Japhet Zabron - Napungukiwa Nini Lyrics
- Song Title: Napungukiwa Nini?
- Album: Nikumbuke
- Artist: Japhet Zabron
- Released On: 19 Mar 2022
- Download/Stream: iTunes Music Amazon Music

Ndege, hawavuni
Hawapandi wala hawafanyi kitu
Mihangaiko, ya dunia sahau wala hawasumbukii
Sauti tulivu
Asabuhi huimba nakushukuru
Wanamjua awapae kuishi kamwe hawahofu kitu
Heeh’ ndivyo aishivyo amtumainie, muumba wa mbingu
Hahangaiki hahofii dunia na masumbuko yajayo
Napungukiwa nini, Napungukiwa nini
Nikiwa naye Yesu
Sina kiu ya kitu
Napungukiwa nini, Napungukiwa nini
Nikiwa naye Yesu
Sina kiu ya kitu
Huna tumaini
Umekwama na kesho inakutisha
Hufika muda
Peke yako, njiani waongea na kulia
Maisha mzigo
Umetengwa wapendwa kukukimbia
Nikukumbushe
Yupo Yesu rafiki hata usiwaze kitu
He he, ndivyo aishivyo
Amtumainie muumba wa mbingu
Hahangaikii hahofii dunia na masumbuko yajayo
Napungukiwa nini (nakosa nini)
Napungukiwa nini (zaidi nini Baba)
Nikiwa naye Yesu
Sina kiu ya kitu
Napungukiwa nini, Napungukiwa nini
Nikiwa naye Yesu
Sina kiu ya kitu
Mungu yupo upande wetu
Nani atakae kaa juu yetu
Tulia, tulia, tuliaa kwa Yesu